Bei ya ndizi soko la MABIBO yapanda

Bei ya ndizi soko la MABIBO yapanda
Bei ya ndizi katika soko la ndizi la mabibo urafiki jijini DSM, imepanda na mkungu mmoja unauzwa kwa kati ya shilingi ELFU 10 hadi shilingi elfu 20 ukilinganisha na hapo awali, mkungu uliuzwa kwa kati ya shilingi LEFU 7 na shilingi ELFU 10.

Mwenyekiti wa soko hilo KIBWANA PAZI amesema kupanda kwa bei kunatokana na uhaba wa bidhaa hiyo msimu huu wa kilimo ambapo kwa sasa zinaingia roli 5 hadi 6 ukilinganisha na roli zaidi 8 kwa siku ilivyokuwa hapo awali.

Post a Comment

0 Comments