BABY MADAHA ANASWA NA MCHEPUKO

BABY MADAHA ANASWA NA MCHEPUKO

Baada ya hivi karibuni kunaswa chobingo akiwa na mwanamuziki Haroun Kahena ‘Inspector Haroun’, mwanadada asiyekaukiwa na vituko Baby Joseph Madaha juzikati alibambwa tena akichezewa kimahaba na njemba ndani ya gari kiasi cha kuwafanya wadau kuhoji, yeye ni cha wote?. 
Baby Joseph Madaha akichepuka na njemba.
Tukio hilo lilijiri hivi karibuni katika Pub moja iliyopo Kijitonyama jijini Dar ambapo mastaa kibao hukutana na kuponda raha. Awali, Baby Madaha alionekana akiwa anapiga ulabu huku akichezea simu yake lakini baada ya muda alinyanyuka na kuelekea kwenye gari iliyokuwa imepaki gizani, ndani kukiwa na mwanaume.
Baada ya paparazi wetu kuusoma mchezo, alilifuata gari hilo na kuwakuta wawili hao wakifanya yao na ndipo zoezi la kuwafotoa lilipoanza. 
Baby Madaha akikurupuka kuzikimbia kamera.
Wakati paparazi akitekeleza jukumu lake, Baby Madaha alianza kubwatuka na kutaka asipigwe picha huku akikimbia kuelekea nyuma ya pub waliyokuwa wakinywa.
Hata hivyo, baada ya Madaha kukimbia paparazi wetu alimfuatilia mwanaume aliyekuwa na mrembo huyo na kugundua kuwa alikuwa ni msanii wa Bongo Fleva anayefahamika kwa jina la Pasha.

Post a Comment

0 Comments